Mafua yasababisha vifo vya watoto 22 Marekani


Watoto 22 wameripotiwa kupoteza maisha kutokana na ugonjwa wa mafua nchini Marekani.

Kwa mujibu wa habari,msimu wa mafua ulianza toka Oktoba 2017 na kuwasumbua wengi nchini humo.

Madaktari wamekuwa wakitibu wagonjwa wa mafua  na kusema kuwa wameongezeka wiki lililopita.

Watu zaidi ya 60 walikuwa wakipelekwa hospitali kutokana na mafua ndani ya wiki moja.

Hata hivyo madaktari wanatumaini kipindi cha watu kuugua mafua nchini humo kinafikia kileleni.

Comments