CHANJO YA SARATANI


NA   MWANDISHI WETU

Zaidi ya wasichana Laki sita na Elfu kuma na sita ( 616000  )wenye umri wa miaka 9 mpaka 14 wilayani kahama mkoani shinyanga wanatarajiwa kupatiwa chanjo ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi  kwa mwaka huu 2018.

Yamebainishwa hayo na mkuu wa wilaya hiyo bwana Fadhili Nkulu kwenye uzinduzi wa chanjo hiyo mpya ambapo  kiwilaya umefanyika katika hospitali ya wilaya kwa lengo la kuwakinga wasichana dhidi ya madhara mbalimbali ya kiafya huku akiwataka viongozi wa serikali,kisiasa,dini,wananchi,wazazi na walezi kuendelea kutoa elimu juu ya chanjo hiyo muhimu kwa jamii.

Kwaupande wake mratibu wa shughuli za  chanjo katika halmashauri ya mji wa kahama bwana Mkola Vedasto amesema chanjo hiyo haina madhara ya aina yoyote kwa mabinti hao hivyo wazazi na walezi wasiwe na hofu juu ya chanjo hiyo kwa watoto wao.


Baadhi ya wasichana waliofika katika uzinduzi huo kupatiwa chanjo hiyo wameuuliza maswali juu ya chanjo hiyo na umuhimu wake kwa mratibu wa chanjo.


Nao wadau mbalimbali waliofika katika zoezi hilo wakiwemo waalimu, manes na wafanyakazi wa idara mbalimbali wameelezea jinsi ambavyo wameweza kufurahishwa na zoezi huku wakliahidi kuendelea kuwa mabalozi wazuri juu ya kampeni hiyo muhimu.

INSERT    WALIMU.

Comments